Andeoli - Wikipedia, kamusi elezo huru
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Andeoli (alifariki Bergoiata, Viviers, 208) alikuwa Mkristo kutoka Smirna (leo nchini Uturuki) aliyefanua umisionari huko Galia (leo Ufaransa) hadi alipouawa wakati wa dhuluma ya kaisari Septimius Severus.
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.
Sikukuu yake huadhimishwa kila tarehe 1 Mei[1].
Andeoli alizaliwa Smirna katika karne ya 2. Akiwa shemasi, alitumwa na askofu Polikarpo,[2] kuinjilisha Galia Kusini pamoja na Benignus.
Kati ya waliowaongoa, mmojawao ni Sinforiani wa Autun, baadaye mfiadini.
Andeoli aliendelea hadi Vivarais alipouawa kwa upanga.[3]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- ↑ Martyrologium Romanum
- ↑ Monks of Ramsgate. "Andeolus". Book of Saints, 1921. CatholicSaints.Info. 19 July 2012
- ↑ Goyau, Georges. "Viviers." The Catholic Encyclopedia Vol. 15. New York: Robert Appleton Company, 1912. 12 April 2020
![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |