sw.wikipedia.org

Wasomali - Wikipedia, kamusi elezo huru

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Wasomali
Soomaali
صوماليون
Maeneo penye idadi kubwa kiasi
Pembe ya Afrika
Lugha

Kisomali

Dini

Karibu wote: Uislamu (Sunni, Sufi)
Wachache pia: Shia, Ukristo au Ukanamungu

Ramani ya koo.

Wasomali ni kabila kubwa la watu wa jamii ya Wakushi wanaoishi katika eneo linaoitwa Pembe ya Afrika ambalo ni eneo linalopakana na Bahari ya Hindi na kugawanyika kati ya nchi asili nne: Somalia, Kenya, Ethiopia na Jibuti.

Idadi ya Wasomali walioko Somalia ni kama milioni 15, Ethiopia milioni 8.5, Kenya ni karibu milioni 2.5 au 3 [1] na Jibuti zaidi ya nusu milioni. Walioko nje ya eneo asili pia ni wengi, hasa huko Yemen. Jumla yao ni milioni 28-30.

Lugha yao ni Kisomali, mojawapo kati ya lugha za Kikushi.

Dini yao ni Uislamu.

  1. kufuatana na takwimu zilizotolewa na Kenya National Bureau of Statistics, Census Bureau
Makala hii kuhusu utamaduni wa Kenya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wasomali kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.